Kaziba : Mwanabunge Félicité Kabonwa Naweza anatakia wakaaji Heri ya Mwaka mupia wa 2024

Kaziba : Mwanabunge Félicité Kabonwa Naweza anatakia wakaaji Heri ya Mwaka mupia wa 2024, wa Umoja, Amani na Maendeleo.Kazibaonline.com au cœur de l’Actualité

Katika Salamu yake yakutakia Heri ya Mwaka mupya kwa Wakaaji wote wa Kaziba, Mwanabunge Pia Régente mustafu wa mukowa wa Kaziba, Mama Felicité Kabonwa Naweza anatakia Heri ya Mwaka mupya kwake baba Mheshimiwa Mwami Majiri IV Dirck N’nakaziba na kwa Wakaaji wote kwa Ujumla.
Mheshimiwa Kabonwa Naweza Félicité amekuwa mwalikwa wa Huduma ya Uandishi ya Kazibaonline.com:

Baba Mwami Majiri IV Dirck, wa baba, wa mama na vijana ninawasalimu nakuwatakiya mwaka mupia wa 2024, wa Amani na Maendeleo. Kulingana na hiyo, Mungu atuwezeshe sote kuishi tena umoja sawa mtu moja kamaa ilivyokuwa zamani. Muzibaziba alikuwa mtu moja, na huo umoja wetu umetuleteya heshima kwa watu wote hata wengine walijuwa kwamba kama unagusa muzibaziba unagusa Umoja wa Wazibaziba yote. Kama Mwami Pamoja na Washemuka wake walikamata hatuwa Fulani, watu wote hata vijana walitii na kuheshimu. Mushangao nikwamba kwa sasa tumepoteza ile umoja yetu, watu hawatii tena wazazi hata na Mwami.

Chombo muzungu alifanya kwa kusaidia, leo imegeuka kuwa njiya ya matusi na matengano. Ninataja Radio na simu yamukononi Ama Téléphone. Tumefata maneno mengi mbele ya uchaguzi na tuliwaza kama hayo yatapita nyuma kumaliza huo uchaguzi na zaidi ingawa Mwami alihamakiya hiyo lakini inaonekana vijana wetu na wazazi wamoja hawasikiye tena sauti ya Mwami, wala kuheshimu haki ya wengine. Kulingana na hiyo yote, mimi sawa mwanabunge wenu na kiongozi honoraire wa chefferie yetu, nimetowa azimiyo hizi kwa viongozi yetu wa chefferie ya Kaziba na wale wanalinda usalama wa watu:

  • Kuhamakiya na kusimamisha kwa muda vipindi vya Politique Ama siasa za uchonganishi kwa Radio za chefferie tukitaja (RTNK na Radio Umoja FM).
  • Kufanya identification ya wasimamizi wa vikundi vya Réseaux sociaux nikitaja Kaziba Débout zote na kila ingine groupe yenyekua na muradi ya Kuzorotesha Amani, kuelimishwa kujuwa ku censurer messages mbaya.
  • Kufanya Utafiti ilitujuwe kupana malipizi kwa vijana fulani ambao ni wachochezi nawenye kutoa maneno mabaya ambayo inaenda kinyume ya sheriya, sanasana Wale vijana walio endesha vurugu, wamoja walileta fujo kwakupiga wengine kwa Makesha ya Uchaguzi tarehe 19 December na siku ya Uchaguzi tarehe 20 December 2023.
  • Viongozi wa groupes WhatsApp washurutishwe Kuondoa wale vijana ambao wanaficha nyuso na majina zao katika vikundi vya WhatsApp,
  • Wale vijana ambao wanaishi inje ya Kaziba, pia inje ya inchi ambao wanaendeleya Kuleta habari za uchochezi wasimamishwe kwa muda ndani ya groupes hizo.
    Tuendeleye pamoja Kufanya Miradi ya Maendeleo katika kuboresha Chefferie yetu, kwamufano kutiya mawe kwa tronçon yakwa Cikara nakwa Cihanza ili safari ya Kwenda Kaziba iwe raisi.
    Aksanti na sisi sote tubaki kimya tukilinda umoja wetu na kumheshimu Mwami wetu pamoja na washemuka wake. Mwaka 2024 Uwe Mwaka wa Umoja, Amani na Maendeleo Kwa wote.” Ni Ujumbe wahii Juma tano tarehe 10 January 2024 Wake Mheshimiwa Félicité Naweza M’KABONWA, Mwanabunge Jimboni Kivu ya Kusini.

Un Peuple, Une Histoire

Charles Irenge Lwaboshi
A propos Charles Irenge Lwaboshi 1310 Articles
Charles IRENGE LWABOSHI est né à Kabembe le 25/05/1991. Fils de LWABOSHI MUTALYA Daniel et de FAIDA M'NANGANDO. Études faites et expériences profesionnelles : (1) Détenteur d'un diplôme d'état obtenu à l'Institut Namurhera de Kaziba INAKA; (2) Détenteur d'un diplôme de Graduat en Sciences Commerciales et Comptable à l'Institut Supérieur de Management ISM Bukavu; en 2010-2018: Journaliste chef des programmes à la Radio Umoja FM de Kaziba; 2013-2017: Enseignant à l'Institut CIMANYE II; 2018 à nos jours il travaille comme journaliste attaché de presse à l'Université de Kaziba; 2019 à nos jours il est directeur à la Radio télévision Ngoma ya Kivu RTNK KAZIBA. Actuellement: il es 1er Vice président territorial de Parlement de Walungu; il est président du Syndicat des Jeunes pour le développement de Kaziba dans le groupement de KABEMBE. Formation: Formation sur la Gestion des radio communautaires par le Centre Lokole; Renforcement de capacité des journalistes par le bureau de communication de la Monusco; Formation en informatique par le Centre de formation GlabalTech; Formation sur le journaliste sensible aux conflits par le DEUTCH VELÉ. Charles est marié à NZIGIRE YSEULT depuis 2013.

Soyez le premier à commenter

Laisser un commentaire